Uwekezaji katika Uchumi wa Nishati Endelevu wa Tanzania

11 - 12 Septemba 2024
Dar es Salaam, Tanzania

Kuwa sehemu ya simulizi ya mafanikio ya ukuaji wa Nishati Tanzania

Jihakikishie nafasi ya kushiriki leo

900

Kilomita za mraba za Eneo la Maonesho

900

Wajumbe

125

Makampuni yaliyofanya maonesho

100

Watoa mada kutoka Wizarani, Serikalini, Wanatasnia

40

Nchi zilizowakilishwa

Karibu katika Mkutano wa Nishati Tanzania 2024

Kufuatia mafanikio ya Mkutano wa Nishati 2023, wandaaji wenza wa Mkutano wa Nishati ambao ni dmg Events na Ocean Business Partners Tanzania, wanayofuraha kukutangazia kuwa Mkutano wa 6 wa Madini Tanzania umeidhinishwa rasmi na  utafanyika jijini Dar es Salaam kuanzia tarehe 11 – 12 Septemba 2024.

Tanzania inaendelea kukua kwa kasi kama nchi wezeshi ya kimkakati katika fursa mpya za kibiashara kwenye tasnia ya nishati Afrika Mashariki. Mwaka huu Mkutano utajikita katika kutoa mrejesho kuhusu maeneo muhimu ya sekta ya nishati Tanzania ikiwa ni pamoja na Mradi wa Kuchakata na Kusindika gesi Asilia (LNG),  mradi wa Bomba la Mafuta Ghafi la Afrika Mashariki (EACOP), Maendeleo ya gesi ya mkondo wa juu,  pamaoja na mapendekezo mbalimbali ya miradi ya nishati jadidifu.

Ungana na wadau muhimu wa ndani, wa kikanda na wa kimataifa Septemba hii ili uwe sehemu ya simulizi ya mafanikio katika ukuaji wa nishati Tanzania.

Waheshimiwa na Viongozi wa Tasnia waliowahi kushiriki

Kuwa sehemu ya simulizi ya mafanikio ya ukuaji wa Nishati Tanzania

Pata maoni kutoka kwa washiriki wa nyuma

“Ushiriki wetu katika mkutano ulituwezesha kubadilishana uzoefu juu ya mada mbalimbali zilizojadiliwa, kujenga mitandao na kuanzisha ubia mpya na washiriki kadhaa. Vile vile, tuliweza kusajili washiriki wapya. Aidha, ilikuwa ni fursa ya kujifunza kwetu hasa juu ya uandaaji wa mikutano na juu ya teknolojia mpya zinazoibuka katika tasnia ya nishati safi na hii ni pamoja na uendelezaji wa nishati ya jotoardhi, hidrojeni safi, na juhudi za kupunguza hewa ukaa katika shughuli za uchimbaji madini, sekta ya uchakataji mafuta na gesi ghafi. Kwa ujumla, mkutano ulikuwa wa thamani kubwa sana kwa shirika letu.”

“Nilishiriki katika hatua zote za hotuba, mawasilisho na chakula cha jioni Serena ambacho kilifadhiliwa na Equinor & Shell. Mkutano mzima uliandaliwa vizuri na hongera kwa timu nzima!”

“Kwakweli, ulikuwa ni mkutano ulioandaliwa vizuri! Tulifanikiwa kukutana na wadau wote tuliotegemea kukutana nao. Hata hivyo, mkutano ulitupa fursa ya kuonesha kuhusu shughuli zetu na siyo tu kuishia kuziongelea. Fursa za kujenga mitandao wakati wa chakula cha jioni zilikuwa ni nzuri sana na zilituwezesha kuzungumza na watu ambao katika mazingira ya kawaida huwa ni wagumu katika mazingira ya mapumziko.”

Kukutana moja kwa moja na Viongozi wa Tasnia ya Nishati Tanzania